SERIKALI YA VISIWA VYA SHELISHELI KUANZISHA KOZI YA UZAMIAJI

Serikali ya Visiwa vya Shelisheli imesema inatarajia kuanzisha kozi ya Uzamiaji nchini Tanzania kwa kushirikiana na Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) haraka iwezekanavyo
Hayo yamesemwa na Balozi wa Visiwa hivyo Mhe. Maryvonne Pool wakati wa mjadala wa pamoja kati ya wawakilishi kutoka Visiwa vya Shelisheli na watumishi wa Chuo cha bahari Dar es Salaam uliofanyika katika ukumbi wa chuo cha DMI tarehe 27.06.2022
Mjadala huo umelenga kupata uzoefu kutoka kwa wawakilishi wa Visiwa vya Shelisheli kuhusiana na Uchumi wa Bluu hususan shughuli za bahari na uvuvi ambao Visiwa hivyo tayari wameshaanza kutekeleza agenda ya Uchumi wa Bluu katika Taifa lao.
Katika majadiliano hayo, Balozi wa Visiwa vya Shelisheli nchini Tanzania Mhe. amesema nchi yake itaanzisha kozi ya Uzamiaji nchini Tanzania kwa kushirikiana na Chuo cha bahari Dar es Salaam (DMI) ili kuongeza fursa katika tasnia ya bahari.
Balozi wa Visiwa vya Shelisheli (Kusoto) akiweka saini katika kitabu cha wageni
Mkuu wa Chuo cha bahari Dar es Salaam Dkt. Tumaini Gurumo (Kulia) akikaribisha ujumbe kutoka Visiwa vya Shelisheli
Balozi wa Visiwa vya Shelisheli akitambulisha timu ya wataalam aliyoambatana nayo
Mtaalamu wa Sheria, Ulinzi na Usalama baharini kutoka Visiwa vya Shelisheli, Bi Sheryl Vangadasamy akitoa mada wakati wa mjadala
Wakuu wa Idara na Vitengo (DMI) wakisikiliza kwa makini